KE

? Furaha, furaha, afya: 1. Amani ya ndani. 2. Kupata kuridhika kutokana na kusaidia na kuwa tegemeo kwa Wengine. Mahusiano. 12R.tv❌✅ Nakutakia Wewe, Mimi na Wengine kwamba mwisho wa mwaka ujao, kila mmoja Wetu aseme: “2022 ulikuwa mwaka bora zaidi wa maisha yangu ??”. Marcin Ellwart

Furaha

Furaha ni mojawapo kati ya maono ya msingi, pamoja na pendo, hamu, chuki, hofu, huzuni na hasira. Furaha inapatikana pale ambapo umepata kile ulichokipenda na ulichokuwa na hamu nacho.

Neno hili tunaweza kutumia katika hali tofautitofauti. Wapo ambao watalitumia kama jina ila wengine ni hali ya kuwa na amani juu ya ufanyaji wa tendo fulani kwa kuwa hauwezi ukafanya kitu kwa furaha bila ya kuridhia mwenyewe au kuwa na amani nacho. Kwa kufanya hivyo unaweza ukafanya vibaya na kuharibu kabisa. Lakini kama umeridhia nacho, unaweza kufanya kitu hicho kwa umakini na kwa usahihi na unaweza kupendezwa nacho mwenyewe. Kwa mantiki hiyo basi tunaona kwamba katika maisha yetu ya kila siku si vyema kumlazimisha mtu mwingine afanye jambo ambalo hayuko tayari nalo kwa sababu anaweza akafanya kinyume kabisa na unavyotaka na kukusababishia matatizo mengine.

Makala bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari.

Wikipedia.org:

https://sw.m.wikipedia.org/wiki/Furaha

Afya

Afya ni hali ya kujisikia vizuri kimwili, kiakili, kiroho na kiutu bila kusumbuliwa na ugonjwa wowote.

Afya ya binadamu itakuwa njema kama atafuatilia kanuni na taratibu bora za afya. Hiyo inajumuisha mlo kamili, yaani chakula chenye virutubishi vyote, vikiwemo protini, wanga na mafuta (hiyo iwe katika asilimia ndogo sana).

Pia anatakiwa awe msafi mwilini na mazingira yake, kama vile kwa kuoga na kusafisha mazingira yanayomzunguka. Mandhari yenye hewa safi pia husaidia katika kuhifadhi afya ya binadamu katika mwili na akili.

Mazingira mara nyingi huchukuliwa kuwa jambo muhimu katika hali ya afya ya binadamu. Hii inajumuisha mazingira ya asili, mazingira ya kujengwa, na mazingira ya kijamii. Pia mambo kama vile maji safi na hewa, makazi salama, huchangia afya nzuri, hasa kwa afya ya watoto wachanga na watoto.[1]

Utafiti umeonyesha kuwa ukosefu wa maeneo ya burudani husabsabisha kupungua kwa afya na ustawi.[2]

Pia anatakiwa kuwa na afya ya kiroho yaani kuishi kadiri ya mafundisho ya Mwenyezi Mungu kama vile: kupendana na wengine, kuthaminiana na kuacha dhambi: mara nyingi hizo zinadhuru afya ya mwili pia.

https://sw.m.wikipedia.org/wiki/Afya

Nchi huru

Nchi huru ni zile ambazo hazitawaliwi na nchi nyingine. Kauli hiyo haimanishi kwamba wananchi wake ni huru, kwa sababu pengine mfalme au rais ni mwenyeji, lakini anawanyima haki zao kwa kiasi hata kikubwa (ambacho kinaitwa udikteta).

Mara nyingi nchi inajitangaza huru, halafu inatambuliwa na nchi nyingine kuwa hivi. Kama si nchi zote zinatambua rasmi uhuru wake, hali ya kisheria inabaki tata.

Siku hizi duniani kuna nchi huru karibu 200, ya mwisho kutambulika ikiwa Sudan Kusini (2011) na ndogo zaidi ikiwa Mji wa Vatikano (km2 0.44 na wakazi 600 hivi tu).

Hii haiuzii nchi kuingiliwa kwa namna moja au nyingine kama vile katika ukoloni mamboleo.

https://sw.m.wikipedia.org/wiki/Nchi_huru

Kiswahili

Kiswahili ni lugha ya Kibantu yenye misamiati mingi ya Kiarabu (30%), lakini sasa ya Kiingereza pia (10%), inayozungumzwa katika eneo kubwa la Afrika ya Mashariki.

Lugha hii ina utajiri mkubwa wa misamiati, misemo, methali, mashairi, mafumbo, vitendawili na nyimbo. Kiswahili hutumika kufundishia shuleni na kuna vitabu vingi vilivyotungwa kwa kutumia lugha hiyo, vikiwa pamoja na vile vya hadithi, hekaya au riwaya.

https://sw.m.wikipedia.org/wiki/Kiswahili